Mamlaka ya Biblia

“Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”
2 Timotheo 3:16-17

WABAPTISTI  kwa karne nyingi sana wamekuwa wakisisitiza kuwa Biblia ndio kitabu pekee chenye mamlaka juu ya imani na destruri kwa Mkristo. Wamekuwa hawakubaliani kabisa na wale wenye mtazamo tofauti na hilo, wakiwemo mapdre, wafalme, maaskofu, wachungaji na waalimu mbalimbali. Jambo hili ndilo hata limepelekea Wabaptisti wengi kuteswa na kunyanyaswa kutoka kwenye vyombo ya dola mbalimbali na hata makundi mengine ya dini kwa sababu ya kuheshimu mamlaka ya Kiblia.

Wabaptisti huthamini Mamlaka ya Biblia

Kimsingi Wabaptisti wamekuwa wakithamini Biblia kama ndicho kitabu chenye mamlaka kwa ajili ya imani na desturi kwa Mkristo kwa sababu ya asili yake. Wabaptisti wameendelea kusisitiza kwamba asili ya Uungu kwenye Biblia ndio sababu huipa hiyo mamlaka. Hakuna kitabu kingine ambacho kinaweza kufananishwa na Biblia. Biblia ni kitabu cha kipekee kati ya vitabu vyote ambavyo viko na kwamba kimetoka kwa Mungu na ni kinahusu Mungu.

Kufuatia historia yetu, Wabaptisti hawana shida na kukubaliana na Biblia kuwa ndicho kitabu chenye mamlaka kwa ajili ya imani na destrui kutokana na asili ya Uungu. Maandiko yalinukuliwa ili kuhalalisha imani na destruri za Wabaptisti bila kutumia nguvu kubwa ili “kusadiki” asili ya Uungu kwa Biblia.

Hata hivyo, Wabaptisti na wengine wanaweza kudhihirisha ushahidi mbalimbali juu ya Uungu, mamlaka ya asili ya Biblia, kama vile umoja uliomo kwenye Biblia licha ya kusema kwamba iliandikwa na watu mbalimbali miaka mingi iliyopita, ukamilifu wa unabii wa Agano la Kale kama vile maisha na mafundisho ya Yesu Kristo, mafunuo mbalimbali ya Biblia kwa karne na karne, nguvu iliyomo iletayo mabadiliko kwenye maisha na jamii, na msisitizo wa kujirudia mara kwa mara kuwa Biblia ni Neno la Mungu.

Asili ya Mamlaka ya Biblia

Wabaptisti husisitiza kuwa Biblia ni maandiko yaliyo na mamlaka juu ya imani na desturi kwa Wakristo na kukataa maandiko mengine kama vile mapokeo ya imani zingine, ungamo za imani, tamaduni,mafundisho ya wana thiolojia, na matamko mbalimbali ya waanzilishi wa madhehebu mbalimbali yana mamlaka pia. Hata kama Wabaptisti wanaweza kupata faida fulani kwenye hayo maandiko, lakini hawakubaliani kabisa kuwa yana mamlaka kwao zaidi ya Biblia.

Wengine wamefikia hatua ya kuwalaumu Wabaptisti kwa kile wanachodhani wanaiabudu Biblia kwa sababu ya ile heshima kubwa ambayo huipa Biblia. Kiuhalisi, hatuiabudu Biblia kama Biblia; tunamwabudu Mungu wa Biblia kama mwenye mamlaka ya mwisho. Biblia inamamlaka kwetu kwa sabau inatoka kwa Mungu na ni ya Mungu mwenyewe.

Hii ndio sababu pekee kwa nini Wabaptisti huthamini sana kuwa Biblia ndio andiko pekee  lenye mamlaka. Mungu ndiyo mwenye mamlaka ya mwisho. Roho Mtakatifu aliwapa uweza wanadamu ili waweze kuiandika Biblia kwa kusudi, kama vile Imani na Ujumbe Wabaptisti huelezea, ni maagizo sahihi ya Kimungu, yana Mungu kama mwasisi wake, wokovu wa milele, ukweli, haina makosa, jinsi ilivyo ni sahihi kabisa. Kwa maana hiyo, Biblia ni ufunuo kutoka kwa Mungu kwetu sisi.

Yesu Kristo ni ufunuo ulikamilika kutoka kwa Mungu. Biblia inamwelezea Yesu kama Bwana wa vitu vyote. Yesu kama Bwana na kusema  Biblia ina mamlaka, hivi vyote huenda sambamba; havipingani kamwe bali husaidiana.

Wabaptisti huamini kwamba ni Roho Mtakatifu aliwasaidia watu kuandika ukweli kuhusu Mungu lakini sio hilo tu bali pia husaidia watu kuelewa na kugundua ukweli uliomo kwenye Biblia.

Kimsingi Biblia ina mamlaka kwenye dini. Herschel Hobbs, Mchungaji marufu wa Baptist-mwanatheolojia, kwenye kitabu kiitwacho The Baptist Faith and Message(Imani ya Baptist na Ujumbe wake) kwenye kurasa 24 – 25 anasema, “Kimsingi Biblia ni kitabu cha dini.”  Anafafanua, “Kusema Biblia ni kitabu chenye mamlaka haina maana kwamba kina mamlaka kwenye kila wazo la mwanadamu, hakina mamlaka kwenye masuala ya sayansi. Hakisemi hivyo.” Hobbs  pia aliandika, hakuna mahali Biblia inaelezea kuwa ni kitabu cha hadithi tu, fasihi, falsafa, saikolojia au sayansi. Japo ni kweli imesheheni mambo mengi yanayofanana na hayo na mengine mengi”

Mamlaka ya Biblia ni sawa na Baadhi ya Mambo ya Msingi ya Imani ya Wabaptisti

Kwa sababu Wabaptisti huamini kuwa Biblia ndio kitabu chenye mamlaka kwa ajili ya imani na desturi, Biblia ndio msingi wa mafundisho na mwenendo wa Baptist. Matamko mbalimbali yaliyopo ya imani ya Baptist kwa karne nyingi yamechukuliwa kwenye Maandiko Matakatifu.

Suala la Mamlaka ya Biblia, Wabaptisti huamini kwenye masuala ya msingi kama vile wokovu hupatikana kwa neema kwa njia ya imani tu, ukuhani wa muumini, uweza wa roho, ubatizo wa muumini, maana ya ubatizo kama mfano na meza ya Bwana, ushirika wa muumini ni kwa wale waliozaliwa mara ya pili tu, uongozi ndani ya Kanisa la mahali, uhuru wa Makanisa, uhuru wa kuabudu, na uhiari wa kujitoa kwa ajili ya huduma na umisheni.

Baadhi ya haya mafundisho na imani huonyesha ni jinsi gani wa Baptist huichukulia Biblia na kuifafanua. Kwa mfano, kuamini katika uweza wa roho na ukuhani wa muumini kwa kila mshirika humfanya kila Mbaptisti anao uwezo wa kuisoma na kuilewa Biblia na kwa kutoa nafasi na wajibu wa kila muumini kwa kuitafsiri na kuielewa bila kufanyiwa hivyo na wengine. Sambamba na hilo, Wabaptisti husisitiza kwamba hakuna mtu au kikundi cha watu chenye mamlaka ya kushawishi ni kipi wanapaswa kukiamini na kufuata.

Baptist husisitiza kwamba kila mtu binafsi anao uhuru wa kumiliki, kusoma na kuitafakari Biblia. Kwa kusimama kwenye msingi wa maisha na mafundisho ya Yesu,Wabaptisti huamini kuwa suala la imani sio la kuingiliwa kila mmoja anao uhuru na asiwepo wa kuingilia imani ya mwingine. Na hata ufafanuzi wa aina yeyote kutoka kwenye Biblia usichukuliwe kwa mwingine.

Kutafsiri mafundisho ya Biblia

Kuna hatari yeyote ambayo yaweza kutokea kwa kila muumini kuitafsiri Biblia akiwa mwenyewe? Ndio, kuna hatari, hatari, hata tafsiri za ajabu sana zinawezo kujitokeza kwa sababu sio kila Muumini amekomaa kwenye Ukristo au kwamba anao utashi wa kutosha kwenye kuitafsiri Biblia.

Lakini kinyume chake ndio hatari zaidi: kuamini kwamba ni watu wachache tu ndio wenye uweza na mamlaka ya kuitafsiri kile ambacho Biblia inafundisha. Zaidi ya hilo, ni nani mwenye mamlaka hayo ya kumpa mtu au kikundi fulani? Kwa kuongezea, wakufunzi wa Biblia hutofautiana sana kwenye kuitafsiri Biblia kwenye baadhi ya maeneo. Ni nani mwenye maamuzi ya kusema hizi tafsiri ziko sahihi?

Hii ina maana kwamba kila mmoja anao uhuru wa kuamini kile anachodhania ni sawa juu kulingana na Biblia na mafundisho yake?  Wabaptisti wao wanasema wako huru kufanya hivyo, lakini hii haina maana kwamba kila tafsiri iko sahihi. Wabaptisti husisitiza kwamba wajibu mkubwa ni kutokana na uhuru uliopo kwenye kuitafsiri Biblia. Watu wanapaswa kuwa waombaji wanapoisoma Biblia, wanyenyekevu, na kutegemea mwongozo wa Roho Mtakatifu. Tafsiri mbalimbali tunapaswa kushirikisha wapendwa wenzetu na waumini ili kupata maarifa zaidi na uelewa. Tafsiri zenye tija zinapaswa kutumika, ni vema ukafananisha tafsiri uliyojifunza na tafsiri za Wakristo waliokomaa, waliopita na hata wa sasa ili kuweza kupata uelewa zaidi juu ya kile ulichokitafsiri.

Hitimisho

Wabaptisti hutofautiana kwenye maeneo mbalimbali kuhusiana na Biblia. Hata hivyo, Wabaptisti wakiwa na tofauti kwa baadhi ya mafundisho na destruri, hutumia Biblia kama chombo chenye mamlaka, na sio njia zingine. Kwa hiyo, hata kama Wabaptisti wanaweza kutofautiana juu ya mafundisho fulani ya Biblia na desturi, tunaamini kuwa Biblia ndio andiko la mwisho juu ya imani na desturi.

“Tunaamini Maandiko kwenye Agano la kale na Agano jipya kwamna ni mafunuo kutoka kwa Mungu, na yaliyo na kweli thabiti yake juu ya imani na mwenendo.”
kutoka kwenye chapisho la Imani huko Texas mnamo mwaka 1840 na Ushirika wa Majimbo ya Baptist